Mkazi wa mtaa wa Mageuzi, kata ya Ngokolo, Shinyanga, Ibrahimu Daniel
(42) amemuua mke wake, kwa kushindwa kuhifadhi vizuri kachumbari na
kupika mboga isiyo na kiwango.
Aliyeuawa ni Stella Ibrahimu (39) na alipigwa baada ya mumewe Daniel
kurudi nyumbani na kuuliza kachumbari ambayo alikula jana yake ndipo
mtoto aliyekuwa akimlea Elizabeth Ibrahimu (13)
alipomuonesha, lakini
hakuridhika nayo na kuanza kuuliza maswali kwa nini haikuhifadhiwa
vizuri.
Waandishi wa habari waliofika eneo la tukio walielezwa na mtoto wa
marehemu, Daniel Ibrahimu (12) kuwa baba yake alipofika nyumbani saa
moja usiku alimkuta yeye akiwa na Elizabeth ndipo alipoanza kumhoji
Eliza akimuuliza kachumbari yake iko wapi.
Daniel alisema baada ya Eliza kumuonesha baba yake kachumbari hiyo
aliyoila na kuibakisha Jumatatu wiki hii, aliiona imechacha na kuonekana
na uchafu, ndipo alitoka nje na kuchukua fimbo anayoihifadhi juu ya
nyumba na kutaka kuanza kumpiga lakini kabla ya kumpiga mtoto huyo
alichoropoka na kukimbia nje.
Aliendelea kusimulia kuwa baada ya kukimbia na binti huyo, mama yake
ambaye alikuwa kazini alifika nyumbani wakati huo mfarakano ukiendelea
na alimkuta baba yao akifoka na baada ya kuuliza kuna nini, aliambiwa
kwa nini hakupika mboga yenye kiwango na kwa nini alipika ugali mwingine
wakati kulikuwa na ugali uliobaki mchana.
“Mama alifika na kuanza kunywa chai lakini baba aliendelea kufoka
ndipo mama alimjibu kwa hasira ndipo alipomuuliza baba uliacha fedha ya
matumizi ya kuweza kupika mboga yenye kiwango, alianza kumpiga baadaye
alimpiga na kikombe na mateke akaanguka ndipo mimi nilikimbia kwa
majirani kuwataarifu mama anapigwa, walikuja na kukuta mama ameanguka
chini baba akiwa anamruka ruka,” alisema Daniel.
Aliyeuawa ni Stella Ibrahimu (39) na alipigwa baada ya mumewe Daniel
kurudi nyumbani na kuuliza kachumbari ambayo alikula jana yake ndipo
mtoto aliyekuwa akimlea Elizabeth Ibrahimu (13) alipomuonesha, lakini
hakuridhika nayo na kuanza kuuliza maswali kwa nini haikuhifadhiwa
vizuri.
Waandishi wa habari waliofika eneo la tukio walielezwa na mtoto wa
marehemu, Daniel Ibrahimu (12) kuwa baba yake alipofika nyumbani saa
moja usiku alimkuta yeye akiwa na Elizabeth ndipo alipoanza kumhoji
Eliza akimuuliza kachumbari yake iko wapi.
Daniel alisema baada ya Eliza kumuonesha baba yake kachumbari hiyo
aliyoila na kuibakisha Jumatatu wiki hii, aliiona imechacha na kuonekana
na uchafu, ndipo alitoka nje na kuchukua fimbo anayoihifadhi juu ya
nyumba na kutaka kuanza kumpiga lakini kabla ya kumpiga mtoto huyo
alichoropoka na kukimbia nje.
Aliendelea kusimulia kuwa baada ya kukimbia na binti huyo, mama yake
ambaye alikuwa kazini alifika nyumbani wakati huo mfarakano ukiendelea
na alimkuta baba yao akifoka na baada ya kuuliza kuna nini, aliambiwa
kwa nini hakupika mboga yenye kiwango na kwa nini alipika ugali mwingine
wakati kulikuwa na ugali uliobaki mchana.
“Mama alifika na kuanza kunywa chai lakini baba aliendelea kufoka
ndipo mama alimjibu kwa hasira ndipo alipomuuliza baba uliacha fedha ya
matumizi ya kuweza kupika mboga yenye kiwango, alianza kumpiga baadaye
alimpiga na kikombe na mateke akaanguka ndipo mimi nilikimbia kwa
majirani kuwataarifu mama anapigwa, walikuja na kukuta mama ameanguka
chini baba akiwa anamruka ruka,” alisema Daniel.
Chanzo habari leo.
Picha
No comments:
Post a Comment